Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, kupandishwa vyeo na uteuzi huo umeanza tangu Februari 28, mwaka huu.
Aliwataja walioteuliwa kushika nyadhifa hizo ni Mrakibu wa Uhamiaji (SI) Edward Chogero kuwa Kamishna wa Divisheni ya Fedha na Utawala, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Samwel Magweiga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Udhibiti na Uongozi wa Mipaka na Mrakibu Mwandamizi (SSI) wa Uhamiaji Gerald Kihinga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Pasipoti na Uraia.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni